Customer Registration Agent (14)
- Dead Line: 2026-03-31
Nafasi
Customer Registration Agent (CR Agent)/Wakala Wa Kusajili Wateja Mtandaoni
Idadi
14
Kampuni
ShinePortal Group
Location
P.O.Box 12116
Tabata Kinyerezi, Ilala
Dar Es Salaam, Tanzania
Faida Za Kuwa CR Agent wa ShinePortal
- Mshahara: TZS 500,000 kwa mwezi
- Mkopo: TZS 150,000 kwa wakala mpya ili kukabiliana changamoto za kifedha za mwanzo kama kununua mahitaji ya msingi, usafiri, au vifaa vya kazi.
- Posho: TZS 3,500 kwa siku
- Fursa ya kukuza kipato na kuendeleza taaluma ndani ya kampuni.
- Mazingira bora ya kazi na msaada wa timu ya ShinePortal.
Sifa Za Mwombaji Kwa Nafasi Ya CR Agent
- Waombaji wanapaswa kuwa na angalau elimu ya Kidato cha Nne (Form 4) au zaidi.
- Uwezo mzuri wa mawasiliano kwa Kiswahili (Kiingereza ni nyongeza).
- Nidhamu, uaminifu, bidii na uwezo wa kushirikiana na watu.
- Uwezo wa kufanya kazi kwa malengo (target-based).
- Uzoefu katika kazi za mauzo au huduma kwa wateja ni faida lakini sio sharti.
Majukumu Ya Kazi Kwa CR Agent
- Kukusanya, kujaza na kusajili taarifa za wateja wanaojiunga na huduma zinazotelewa na kampuni
- Kuhakikisha usahihi wa taarifa na nyaraka za wateja
- Kukagua na kuthibitisha uhalali wa vitambulisho na nyaraka zinazohitajika
- Kutoa maelezo na miongozo sahihi kuhusu mchakato wa usajili na huduma zinazotolewa na kampuni
- Kuingiza taarifa za wateja kwenye mifumo ya kidijitali kwa usahihi
- Kufanya kazi kwa kuzingatia sera, taratibu na maadili ya taasisi
- Kushirikiana na idara nyingine husika kama idara ya Mikopo, Uwekezaji, HR na Huduma kwa Wateja
- Kuandaa na kuwasilisha ripoti za kazi za kila siku, wiki au mwezi
- Kuhudumia wateja kwa heshima, uadilifu na weledi wa hali ya juu
Mshahara Na Motisha
- Mshahara wa msingi ni TZS 500,000 kwa mwezi
- Mshahara huu unajumuisha bonasi na/au posho kwa kuzingatia uzoefu na ujuzi wa mwombaji pamoja na kiwango cha matokeo ya kazi kama itakavyoainishwa kwenye mkataba rasmi wa ajira
Jinsi Ya Kutuma Maombi
Kwa utaratibu wa kupokea maombi ya kazi, maombi yote hutumwa kupitia akaunti ya mwombaji. Ili kuendelea, utabofya kitufe cha CONTINUE hapo chini na
Kwa utaratibu wa kupokea maombi ya kazi, maombi yote hutumwa kupitia akaunti ya mwombaji. Ili kuendelea, utabofya kitufe cha CONTINUE hapo chini na
kisha:-
- Uta Login kwenye akaunti yako kama tayari una akaunti au
- Uta Create akaunti kama bado huna akaunti
Kumbuka,
- Nambari ya simu utakayotumia kufungua akaunti ndiyo itakayotumika kukutumia majibu ya maombi yako kwa SMS au simu, hivyo hakikisha unaweka nambari sahihi na inayopatikana.
- Tengeneza password utakayoikumbuka, kwani utaitumia kila unapologin kwenye akaunti yako.
- Hakikisha password yako ina character 8 au zaidi
Baada ya kulogin au kucreate akaunti, tafadhali rudi tena katika ukurasa huu na ubofye tena kitufe cha CONTINUE, ili uweze kujaza fomu ya maombi na kutuma ombi lako.